Wadau zao parachichi waahidi kuliongezea thamani

By Elizabeth John , Nipashe Jumapili
Published at 03:04 PM Jan 18 2026
Wadau zao parachichi waahidi kuliongezea thamani
Picha: Elizabeth John
Wadau zao parachichi waahidi kuliongezea thamani

Jumuiya ya Wadau wa Parachichi Tanzania (ASTA), kupitia Mwenyekiti wake mpya, imesema itahakikisha inasimamia kikamilifu mchakato wa ujenzi wa kiwanda kipya cha kuchakata mafuta yatokanayo na zao hilo, hatua itakayosaidia kuongeza thamani.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wadau wa Parachichi Tanzania (ASTA), Emmanuel Kisinda, wakati wa mkutano wa jumuiya hiyo uliofanyika Halmashauri ya Mji Njombe.

Kisinda amesema kuwa jumuiya hiyo imelenga kuhakikisha kiwanda cha kuchakata parachichi kinajengwa ndani ya mwaka 2026. 

Aidha, amebainisha kuwa ASTA itaendelea kuhamasisha ongezeko la wanachama, kwa sasa jumuiya hiyo ina wanachama wasiopungua 3,000 wakiwamo wakulima, ili kuongeza uelewa kuhusu ASTA na majukumu yake.

Wadau zao parachichi waahidi kuliongezea thamani
Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe, Zacharia Mwansasu, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka, amesema serikali imeendelea kufanya juhudi mbalimbali kuhakikisha zao la parachichi linapata thamani zaidi sokoni.