slot gacor
slot gacor
slot gacor
Norway yavutiwa kuwekeza biashara Kaboni | Nipashe

Norway yavutiwa kuwekeza biashara Kaboni

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 07:27 PM Jan 29 2026
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Hamad Yussuf
Massauni (kushoto) akizungumza na Balozi wa Norway Nchini Tanzania
Tone Tinnes walipokutana ofisi kwake Dodoma, Januari 29, 2026.
Picha: Mpigapicha Wetu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Hamad Yussuf Massauni (kushoto) akizungumza na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Tone Tinnes walipokutana ofisi kwake Dodoma, Januari 29, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Tone Tinnes, katika ofisi yake jijini Dodoma, Januari 29, 2026, ambapo wameonesha nia ya kuimarisha ushirikiano na kuwekeza katika Biashara ya Kaboni.

Katika mazungumzo hayo, Masauni amemshukuru Balozi Tinnes kwa kuendeleza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Norway na Tanzania, huku akieleza kuwa Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) kinaendelea kuimarika kadri siku zinavyosonga mbele, hatua inayoongeza ufanisi katika usimamizi wa biashara hiyo.

Aidha, Waziri Masauni ameeleza mpango wa Serikali wa kutoa elimu kwa umma kuhusu Biashara ya Kaboni kuanzia ngazi za juu hadi kwa wananchi wa kawaida, lengo likiwa ni kuwezesha makundi mbalimbali ya kijamii kuchangamkia fursa zinazopatikana katika sekta hiyo muhimu.

Pia ameongeza kuwa Taifa linaendelea kujidhatiti katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kama mojawapo ya mikakati ya kulinda na kuhifadhi mazingira nchini, sambamba na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.