slot gacor
slot gacor
slot gacor
Watoto 8,300 waandikishwa darasa la awali Mbeya | Nipashe

Watoto 8,300 waandikishwa darasa la awali Mbeya

By Nebart Msokwa , Nipashe
Published at 06:47 PM Jan 30 2026
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Erica Yegella

Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, imeandikisha zaidi ya wanafunzi 8,300 wa darasa la awali kwa mwaka huu wa masomo.

Imeelezwa kuwa kuna ongezeko la mwamko wa wazazi kuwapeleka watoto wao shule.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Erica Yegella ameyasema hayo wakati akizungumza na wandishi wa habari kuhusu uandikishaji wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Amesema kwa darasa la kwanza wameandikisha wanafunzi 900 na kwa kidato cha kwanza wameandikisha wanafunzi 6523 ambao wameandikishwa katika shule mbalimbali za sekondari katika halmashauri hiyo.

Amesema kutokana na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi, halmashauri hiyo imeendelea kutumia mapato ya ndani na fedha kutoka serikali kuu kuboresha miundombinu mipya ikiwemo vyumba vya madarasa, madawati na vyoo.

Amesema ongezeko la wanafunzi wanaoandikishwa  sekondari na msingi linachochewa na vitu mbalimbali ikiwemo sera ya elimu bila malipo kwa sekondari za serikali.