slot gacor
slot gacor
slot gacor
RC aagiza w’biashara wa zamani wapewe kipaumbele soko jipya | Nipashe

RC aagiza w’biashara wa zamani wapewe kipaumbele soko jipya

By Marco Maduhu , Nipashe
Published at 02:21 PM Jan 12 2026
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, akiwa katika soko la maganzo akinunua bidhaa, alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa soko jipya la Maganzo
Picha: Maco
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, akiwa katika soko la maganzo akinunua bidhaa, alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa soko jipya la Maganzo

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Emmanuel Johnson, kuhakikisha wafanyabiashara waliokuwa wakifanya biashara katika soko la zamani la Maganzo, wapewe kipaumbele cha kurejea katika soko jipya, baada ya kukamilika kujengwa.

Ametoa agizo hilo jana, alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa soko la kisasa la Maganzo.

Amesema, wafanyabiashara wa awali ambao walikuwa wakifanya biashara katika soko hili, hao ndiyo wanapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza kuingia katika soko hili jipya.

RC Mahita akiwa kwenye ziara aagiza w’biashara wa zamani wapewe kipaumbele soko jipya
“Ni muhimu wafanyabiashara waliopisha ujenzi wa soko hili, wapewe nafasi za kwanza, sababu hawa ndio walikuwa wakifanya biashara hapa, wakilipa ushuru na kuchangia mapato ya halmashauri, si vyema wakaachwa,” amesema Mhita.

Nao baadhi ya wafanyabiashara hao akiwamo Simon Andrew, wameiomba serikali kukamilisha haraka ujenzi wa soko hilo jipya, ili waondokane kufanya biashara katika mazingira ambayo siyo rafiki.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa soko hilo Hilda Hozza kutoka Mgodi wa Mwadui, amesema linajengwa kwa gharama ya Sh. milioni 260, likiwa na vizimba 200, na hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 70.